Wednesday, February 26, 2014

Magereza mkoa wa Tanga yaanza maandalizi ya ukarabati wa ofisi mpya za utawala

 Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Magereza Edither Malya(wa pili kulia) akielezea hatua mbalimbali za Maandalizi ya ukarabati wa Jengo la Ofisi za Utawala za Magereza Mkoa wa Tanga(wa kwanza kulia) ni Afisa Habari wa Jeshi la Magereza, Mkaguzi wa Magereza Deodatus Kazinja alipotembelea kujionea hatua mbalimbali za ukarabati unaoendelea leo Februari 7, 2014 Jijini Tanga.
Muonekano wa mbele wa Jengo la Kikoloni ambalo linalotarajiwa kukarabatiwa kwa ajili ya Ofisi za Utawala za Magereza Mkoa wa Tanga. Jengo hilo hapo awali lilitumika kama Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Tanga ambapo hivi sasa Jeshi la Magereza tayari limeanza ukarabati wa jengo hilo. Wa kwanza katika picha ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Magereza Edither Malya akiwa ameongozana na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza leo Februari 07, 2014 Jijini Tanga.