Monday, September 29, 2014

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Tanzania ashiriki maadhimisho ya Magereza Day nchini Zambia

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Tanzania, John Casmir Minja(wa tatu kulia) akisalimiana na Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini Zambia, Mhe. Nickson Chilangwa(wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Raphael Hamunyela. Maadhimisho hayo yamefanyika Septemba 26, 2014 katika Viwanja Vya Chuo Cha Maafisa Magereza Mjini Kabwe, Zambia.
Baadhi ya Maafisa na Askari Magereza na wageni wengine Waalikwa wakifutilia matukio mbalimbali yaliyofanyika katika Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia. Maadhimisho hayo yalifanyika katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa na Askari Kabwe, Zambia.

Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja akiongozana na Wakuu Wengine wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Nchini Zambia kuelekea kwenye Jukwaa Kuu kushiriki Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia(wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Raphael Hamunyela.
 
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja(wa Nne kulia Jukwaa Kuu) akiwa na Wakuu Wengine wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Nchini Zambia wakipokea Salaamu ya heshima kutoka kwa Maafisa na Askari Magereza Nchini Zambia(hawapo pichani)wakati Gwaride hilo likipita mbele ya Jukwaa Kuu kwa mwendo wa pole na haraka katika Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia(wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Jeshi la Magereza Nchini Zambia, Kamishna Percy Chato
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja(wa pili kushoto) akiwa na Mkuu wa Magereza Nchini Zambia, Kamishna Percy Chato wakiaangalia kazi za aina mbalimbali zinazofanywa na Wafungwa wa Zambia katika Mabanda mbalimbali kwenye Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia.
 Gadi Maalum ya Maafisa na Askari Magereza wa Nchini Zambia wakipita mbele ya Jukwaa Kuu kwa mwendo haraka katika sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia yaliyofanyika Septemba 26, 2014.
 Kwaya ya Wafungwa wa Nchini Zambia wakitoa Burudani ya nyimbo za Injili wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Magereza Nchini Zambia yaliyofanyika Septemba 26, 2014.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Nchini Zambia, Mhe. Nickson Chilangwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Urekebishaji/Magereza Afrika(walioketi). Wa Nne kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja(wa tano kulia) ni Mkuu wa Jeshi la Magereza Nchini Zambia, Percy Chato(wa tatu kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Raphael Hamunyela(Picha zote na Kitengo cha Habari Makao Makuu ya Jeshi la Magereza).