Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya Twiga Cement, Bw. Alphonso Rodrudges(suti ya bluu) akikabidhi mfano wa hundi yenye kiasi cha Tsh. Millioni Miamoja kwa Uongozi wa Jeshi la Magereza zitakazotumika katika ujenzi wa nyumba zenye hadhi kwa Maofisa na Askari wa Gereza Wazo,Wilayani Kinondoni (wa pili kulia) ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulawakil(wa tatu kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja, (wa kwanza kushoto) ni mtaalam mshauri wa Twiga cement Bw. Saidi Subety. hafla hiyo imefanyika leo Novemba 17, 2014 katika viwanja vya Gereza Wazo, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulawakil hotuba yake fupi katika hafla ya kupokea vifaa vya ujenzi wa nyumba zenye hadhi kwa Maofisa na Askari wa Gereza Wazo,Wilayani Kinondoni, hafla hiyo imefanyika leo Novemba 17, 2014 katika viwanja vya Gereza Wazo, Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi katika hafla ya kupokea vifaa vya ujenzi wa nyumba zenye hadhi kwa Maofisa na Askari wa Gereza Wazo,Wilayani Kinondoni, hafla hiyo imefanyika leo Novemba 17, 2014 katika viwanja vya Gereza Wazo, Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Vifaa vya ujenzi vilivyokabidhi leo na Kampuni ya Twiga Cement. Kampuni hiyo imekabidhi mifuko 1200 ya saruji pamoja na fedha Tsh. Millioni Miamoja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zenye hadhi kwa Maofisa na Askari wa Gereza Wazo,Wilayani Kinondoni.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulawakil(kushoto) akikata utepe kabla ya kukabidhiwa rasmi vifaa vya ujenzi pamoja na hundi yenye kiasi cha Tsh. Millioni Miamoja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zenye hadhi kwa Maofisa na Askari wa Gereza Wazo,Wilayani Kinondoni.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak
Abdulawakil(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi
wa Jeshi la Magereza mara baada ya kukabidhiwa rasmi vifaa vya
ujenzi pamoja na hundi yenye kiasi cha Tsh. Millioni Miamoja kwa ajili
ya ujenzi wa nyumba zenye hadhi kwa
Maofisa na Askari wa Gereza Wazo,Wilayani Kinondoni(wa tatu toka kulia)
ni Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja(wa kwanza kulia) ni
Kamishna wa Magereza Huduma za Urekebishaji, Injinia. Deonice
Chamulesile(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa
Magereza, Dkt. Juma Malewa (wa tatu kushoto) ni Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya Twiga Cement, Bw. Alphonso Rodrudges, (wa pili kulia) ni Mtaalam Mshauri wa Twiga Cement Bw. Saidi Subety.
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la
Magereza).