Friday, December 12, 2014

Makabidhiano ya mkataba wa makubaliano ya mradi wa ubia wa uchimbaji madini ya chokaa kati ya shirika la Jeshi la Magereza na kampuni ya Twiga Cement yafanyika leo jijini Dar

Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja akimkabidhi Mkataba wa Makubaliano ya mradi uchimbaji madini Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Twiga Cement, Bw. Alphonso Rodrudges. Shirika la Magereza limeingia ubia katika mradi huo na Kampuni ya Twiga Cement katika eneo la Jeshi la Magereza, Wazo Hill lililopo jijini Dar es Salaam ambapo hafla hiyo imefanyika leo Desemba 12, 2014 katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja akiwa makini kumsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Twiga Cement, Bw. Alphonso Rodrudges(hayupo pichani) kabla ya makabidhiano rasmi ya Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ubia wa uchimbaji madini ya chokaa. Shirika la Magereza limeingia ubia katika mradi huo na Kampuni ya Twiga Cement katika eneo la Jeshi la Magereza, Wazo Hill lililopo jijini Dar es Salaam ambapo hafla hiyo imefanyika leo Desemba 12, 2014 katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Twiga Cement, Bw. Alphonso Rodrudges(kushoto) akifuatilia majadiliano kabla ya makabidhiano rasmi ya Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ubia wa uchimbaji madini ya chokaa.Shirika la Magereza limeingia ubia katika mradi huo na Kampuni ya Twiga Cement katika eneo la Jeshi la Magereza, Wazo Hill lililopo jijini Dar es Salaam(kulia) ni Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya Twiga Cement.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza waliohuhuria hafla hiyo ya makabidhiano rasmi ya Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ubia wa uchimbaji madini ya chokaa(wa kwanza kulia) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, John Masunga(wa kwanza kushoto) ni Afisa Ugavi Mkuu wa Shirika la Magereza,  Mrakibu wa Magereza, George Wambura

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).