Monday, December 15, 2014

Waandishi wa habari watembelea miradi ya uzalishaji mali ya Jeshi la Magereza mkoani Arusha na Kilimanjaro

Mkuu wa Magereza Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Hamis Nkubas akifanya mahojiano maalum Ofsini kwake  na Waandishi wa Habari kutoka Vyombo vya Habari vya Habari Leo, Daily News, Michuzi Media na Gazeti la Tanzania Daima. Waandishi haowameanza ziara leo Desemba 15, 2014 ambapo watatembelea katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali inayotekelezwa kwa mafanikio na Jeshi la Magereza.
Viti vya Ofisi ambavyo vimetengenezwa katika Kiwanda cha Samani Arusha cha Jeshi la Magereza. Viti hivyo vitatumiwa katika Ofisi za Jimbo kwa Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri  Muungano wa Tanzania.
Viatu vya ngozi vinavyotengenezwa kwa ustadi mkubwa katika Kiwanda cha Viatu vya ngozi cha Gereza Kuu Karanga Moshi kama vinavyoonekana katika picha.
Waandishi wa Habari wakiangalia viatu vya ngozi vinavyotengenezwa katika Kiwanda cha ngozi cha Gereza Kuu Karaga Moshi(wa pili kushoto) ni Mwandishi kutoka Daily News, Bw. Fining Simbeye(wa tatu kushoto) ni Mwandishi kutoka Gazeti la Tanzania Daima, Bw. Edson Kamkara.
Mkuu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Venant Kayombo(wa tano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Waandishi wa Habari kutoka Magazeti ya Daily News, Tanzania Daima, Habari Leo pamoja na Globu ya Michuzi

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).