Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Wednesday, August 13, 2014

Kamishna Generali wa Magereza Nchini akutana na ujumbe kutoka kwa kampuni ya Equator Automech jijini Dar es Salaam

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akisisitiza jambo katika  mazungumzo na Ujumbe Maalum kutoka Kampuni ya Equator Automech inayojishughulisha na uunganishaji Magari na Matrekta hapa Nchini. Kampuni hiyo ipo katika mazungumzo ya Awali ya kuingia Ubia na Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza katika miradi mbalimbali ya Uzalishaji ikiwemo ya Kilimo. Ujumbe huo umefanya mazungumzo hayo leo Agosti 13, 2014 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Equator Automech, Robert Ndege(wa kwanza kushoto) akielezea namna Kampuni yake itakavyoshrikiana na Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza katika miradi mbalimbali ya Uzalishaji ikiwemo ya Kilimo(katikati) ni Mkurugenzi Mshauri wa Kampuni hiyo, Ahmed Bakari akifuatilia mazungumzo hayo.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia mazungumzo ya namna Kampuni ya Equator Automech itakavyoshrikiana na Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza katika miradi yake ya Kilimo. Mazungumzo hayo yamefanyika leo Agosti 13, 2014 Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(katikati) ni Mkuu wa Kitengo cha Kilimo na Mifugo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mlasani Kimaro(wa kwanza kushoto) ni Mthibiti wa Fedha wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Gideon Nkana(wa pili kushoto) ni Mwanasheria wa Jeshi la Magereza, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Issack Kangura(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).


Monday, August 11, 2014

Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa Pension wa PPF afanya mazungumzo ya awali kuhusu uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza mkoa wa Dar es Salaam na Mtwara

 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akiongoza Kikao cha Mazungumzo ya Awali na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio(hayupo pichani) kuhusu Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio akifanya mazungumzo ya Awali na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(hayupo pichani) kuhusu Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara Agosti 11, 2014 Jijini Dar es Salaam.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia mazungumzo ya Awali na Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw William Erio(hayupo pichani) kuhusu Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga(Kushoto) ni Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Magereza, Solomon Urio akifuatilia kwa makini mazungumzo hayo.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(kushoto) akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio eneo linalofaa Uwekezaji wa Hoteli kubwa ya Kimataifa lililopo Ukonga, Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa PPF amefanya mazungumzo ya Awali na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza kuhusu Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza Agosti 11, 2014 Jijini Dar es Salaam
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini John Casmir Minja akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio(kulia) mara tu baada ya kufanya mazungumzo ya Awali kuhusu Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza katika Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara. Mkurugenzi Mkuu wa PPF amefanya mazungumzo hayo  Agosti 11, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).