Wednesday, August 13, 2014
Kamishna Generali wa Magereza Nchini akutana na ujumbe kutoka kwa kampuni ya Equator Automech jijini Dar es Salaam
7:57 PM
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja
akisisitiza jambo katika mazungumzo na Ujumbe Maalum kutoka Kampuni ya
Equator Automech inayojishughulisha na uunganishaji Magari na Matrekta
hapa Nchini. Kampuni hiyo ipo katika mazungumzo ya Awali ya kuingia Ubia
na Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza katika miradi
mbalimbali ya Uzalishaji ikiwemo ya Kilimo. Ujumbe huo umefanya
mazungumzo hayo leo Agosti 13, 2014 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Equator Automech, Robert
Ndege(wa kwanza kushoto) akielezea namna Kampuni yake itakavyoshrikiana
na Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza katika miradi
mbalimbali ya Uzalishaji ikiwemo ya Kilimo(katikati) ni Mkurugenzi
Mshauri wa Kampuni hiyo, Ahmed Bakari akifuatilia mazungumzo hayo.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia mazungumzo ya
namna Kampuni ya Equator Automech itakavyoshrikiana na Jeshi la
Magereza kupitia Shirika lake la Magereza katika miradi yake ya Kilimo.
Mazungumzo hayo yamefanyika leo Agosti 13, 2014 Jijini Dar es Salaam(wa
kwanza kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma
Malewa(wa pili kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza,
Gaston Sanga(katikati) ni Mkuu wa Kitengo cha Kilimo na Mifugo, Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mlasani Kimaro(wa kwanza kushoto) ni
Mthibiti wa Fedha wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Magereza, Gideon Nkana(wa pili kushoto) ni Mwanasheria wa Jeshi la
Magereza, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Issack Kangura(Picha zote na
Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Monday, August 11, 2014
Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa Pension wa PPF afanya mazungumzo ya awali kuhusu uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza mkoa wa Dar es Salaam na Mtwara
8:21 PM
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja
akiongoza Kikao cha Mazungumzo ya Awali na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa
Pensheni wa PPF, Bw. William Erio(hayupo pichani) kuhusu Uwekezaji
katika maeneo ya Jeshi la Magereza Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio
akifanya mazungumzo ya Awali na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza
Nchini, John Casmir Minja(hayupo pichani) kuhusu Uwekezaji katika maeneo
ya Jeshi la Magereza Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara Agosti 11, 2014
Jijini Dar es Salaam.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia
mazungumzo ya Awali na Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw William Erio(hayupo
pichani) kuhusu Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza Mikoa ya
Dar es Salaam na Mtwara(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Sheria na
Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) ni Kamishna wa Fedha
na Utawala, Gaston Sanga(Kushoto) ni Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la
Magereza, Solomon Urio akifuatilia kwa makini mazungumzo hayo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir
Minja(kushoto) akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,
Bw. William Erio eneo linalofaa Uwekezaji wa Hoteli kubwa ya Kimataifa
lililopo Ukonga, Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa PPF amefanya
mazungumzo ya Awali na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza kuhusu
Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza Agosti 11, 2014 Jijini Dar
es Salaam
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini John Casmir Minja
akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William
Erio(kulia) mara tu baada ya kufanya mazungumzo ya Awali kuhusu
Uwekezaji katika maeneo ya Jeshi la Magereza katika Mikoa ya Dar es
Salaam na Mtwara. Mkurugenzi Mkuu wa PPF amefanya mazungumzo hayo
Agosti 11, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es
Salaam(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).