Thursday, March 12, 2015

Magereza Watinga Kilele cha Mlima Kilimanjaro‏

Baadhi ya Maafisa, Askari na Mtumishi raia ambaye pia Mhasibu Mkuu wa Jeshi la Magereza Estomih Hamis  (Mzee wa Magereza Kileleni) wa saba kutoka kushoto wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili katika kilele cha Mlima Kilimanjaro asubuhi ya Machi 9, 2015 na kutundika bendera ya Jeshi hilo kileleni.
Kiongozi wa Msafara wa Maafisa, Askari na baadhi ya watumishi raia wa Jeshi la Magereza waliopanda mlima Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy (kushoto) akikabidhi bendera ya Jeshi la Magereza kwa Mnadhimu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza Dickson Mlay aliyemwakilisha Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro katika kupokea msafara wa wapanda mlima wa Jeshi hilo katika Lango la Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro la Marangu.
Mkuu wa Gereza Kuu la Karanga Moshi Kamishna Msaidizi wa Magereza Dk. Hasan Mkwiche akipokea cheti kutoka kwa Mkuu wa Hifadhi ya Mlima wa Kilimanjaro Ndugu Erastus Lufungulo (wa kwanza kushoto) ikiwa ni ishara ya kuwa amepanda Mlima Kilimanjaro na kufika kileleni. Dk. Mkwiche ni miongoni wa Maafisa wa Magereza 16 waliofika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro cha Uhuru kwa upande wake ikiwa ni mara ya pili kupanda mlima huo kwa mafanikio mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 2011.
Kiongozi wa Msafara wa Maafisa, Askari na baadhi ya watumishi raia wa Jeshi la Magereza waliopanda mlima Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy akiwa katika uso wa furaha mara alipowasili katika kituo cha Gilman’s kabla ya kuanza safari ya kuelekea kilele cha Mlima huo cha Uhuru. Kushoto ni Mkaguzi wa Magereza Bakari Boi akiwa katika sura ya uchovu baada ya safari ndefu ya usiku kucha kutoka Kituo cha Kibo kuelekea Gilman’s.
Wakaguzi wa Magereza Abas Mikidadi (katikati), Jamhuri Yassin (kushoto), Deodatus Kazinja (aliyekaa kulia) na Bakari Boi wakiwa katika sura za uchovu mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Gilman’s  alfajiri ya tarehe 09 Mach, 2015 baada ya safari ndefu na ngumu iliyoanza usiku wa saa tano tarehe 08 Machi, 2015 kutoka Kibo kwenda Gilman’s kabla ya kuhitimisha safari yao katika kilele cha Mlima huo cha Uhuru.
Baadhi ya Maafisa, askari na watumishi raia wa Jeshi la Magereza na wasaidizi wao (guiders)  wakiwa wamepumzika usiku wa manane katikati ya njia ya kutoka Kibo kuelelekea Gilman’s na baadae kilele cha Uhuru. Safari ya kutoka Kibo kwenda Gilman’s  ilianza usiku wa saa 5:13 Machi 8, 2015 na kuhitimishwa Asubuhi ya saa moja Machi 9,2015.
 
Baadhi ya Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika nyuso za furaha baada ya kuwasili katika Kituo cha Horombo kutoka Kituo cha Mandala baada ya kutembea umbali wa kilometa 11 na kulala hapo kabla ya kuanza safari ya kilometa tisa kutoka Horombo kwenda Kibo kesho yake.Kushoto mwenye nguo nyeupe ni Kiongozi wa Msafara Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy na aliyeinua Mkono juu ni Mhasibu Mkuu wa Jeshi la Magereza Estomih Hamis (Mzee wa Magereza Kileleni). Hamis ndiye aliyekuwa na umri mkubwa kuliko wote katika kundi la watu 20 unaokaribia kabisa miaka 60.
Kundi la Maafisa, askari na watumishi raia wa Jeshi la Magereza pamoja wa waongoza njia (guiders) kwa pamoja likiwa katika mwendo wa kilometa tisa kutoka Horombo kwenda kituo cha Kibo ambapo liliwasili majira ya saa tisa alasiri na kupumzika kabla ya kuanza safari ya kwenda Gilman’s saa tano usiku.
Baadhi ya  Maafisa, askari na watumishi raia wa Jeshi la Magereza wakiwa  katika picha ya pamoja baada ya kuwasili katika kituo cha Mandala kutoka Lango Kuu la Marangu. Mandala ni kituo kilicho umbali wa takribani kilometa 8 kutoka Marangu na kiko katika mwinuko wa mita 2720 kutoka usawa wa Bahari.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Venant Kayombo akikabidhi bendera ya Jeshi la Magereza kwa kiongozi wa Msafara wa wapanda mlima wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy katika Lango Kuu la Hifadhi ya Mlima Kilimanaro kabla ya kuanza zoezi la kupanda mlima huo March 6, 2015. 

Picha zote na Mkaguzi wa Magereza Deodatus Kazinja