Monday, May 25, 2015

Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi afungua kikao cha bajeti ya shirika la Magereza kwa mwaka 2015/2016 leo mkoani Morogoro

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(suti nyeusi) akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja mara baada ya kuwasili leo Mei 25, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Edema, Mkoani Morogoro kwa ajili ya ufunguzi wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016(wa pili kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani) kutoa hotuba ya ufunguzi wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016.
Wajumbe wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016 wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi leo Mei 25, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Edema, Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akimkabidhi Begi lenye makabrasha ya Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(wa kwanza kulia) ni  Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016 waliosimama(wa tatu kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(wa tatu kulia) ni  Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa pili kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).