Saturday, June 27, 2015

Rais Kikwete mgeni rasmi siku ya Magereza, afunga rasmi mafunzo ya uofisa ngazi ya juu ya Jeshi la Magereza, jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP), John Casmir Minja akimkarisha Rais Jakaya Kikwete (kushoto) katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kufunga mafunzo ya uofisa wa Cheo cha Mrakibu Msaidizi wa Jeshi hilo. Maafisa 104 wa kozi hiyo walihitimu mafunzo hayo na kuvishwa vyeo hivyo. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP), John Casmir Minja akitoa hotuba yake kabla ya Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani) kuyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi hilo pamoja na kuwavisha vyeo vya Mrakibu Msaidizi wahitimu 104 wa jeshi hilo. Katika hotuba yake CGP Minja alisema jeshi lake linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu mkubwa wa nyumba za askari na maafisa Magereza.
Kikosi cha gwaride wa Askari wa Jeshi la Magereza la zamani (askari jela) likionyesha jinsi kipindi cha zamani jeshi hilo lilivyokuwa linafanya gwaride lake katika sherehe na shughuli mbalimbali za Jeshi hilo. Tukio hilo lilifanyika kabla ya Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani) kuyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi hilo pamoja na kuwavisha vyeo vya Mrakibu Msaidizi wahitimu 104 wa jeshi hilo katika sherehe iliyofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete akikagua gwaride liloandaliwa kwa ajili yake na wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi la Magereza kabla ya kuyafunga mafunzo ya Cheo cha Mrakibu Msaidiziyaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam. Rais Kikwete aliyafunga mafunzo hayo ambayo yalienda sambamba na Siku ya Magereza ambapo alikagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na jeshi hilo nchini.


Rais Jakaya Kikwete (wakumi kushoto-waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Maafisa wa Jeshi la Magereza, wahitimu pamoja na wageni waalikwa, baada ya kuyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi hilo pamoja na kuwavisha cheo cha Mrakibu Msaidizi wahitimu 104 wa jeshi hilo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akitoa hotuba fupi pamoja na kumkaribisha Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani) kwa ajili ya kuzungumza na askari, maafisa wa Jeshi la Magereza pamoja na wageni waalikwa na baadaye kuyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi hilo pamoja na kuwavisha vyeo cha Mrakibu Msaidizi wahitimu 104 wa jeshi hilo. Katika hotuba yake Waziri Chikawe alisema Jeshi hilo linakabiliwa na upungufu mkubwa wa magereza.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia), akimkarisha Rais Jakaya Kikwete kuketi baada ya kukagua gwaride la wahitimu 104 wa kozi ya Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Magereza kabla ya Rais huyo kuyafunga mafunzo hayo katika sherehe iliyofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP), John Minja, na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick.
Rais Jakaya Kikwete akimvisha muhitimu Amina Lidenge, Cheo cha Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Magereza kwa niaba ya wenzake 104 waliomaliza mafunzo hayo katika Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam. Rais Kikwete aliyafunga mafunzo hayo ambayo yalienda sambamba na Siku ya Magereza ambapo baada ya kuyafunga aliweza kutembelea mabanda na kuonyeshwa bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na jeshi hilo nchini.
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Askari na Maafisa wa Jeshi la Magereza, wageni waalikwa na wananchi wakati akiyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshihilo na kuwatunukia vyeo vya Warakibu Wasaidizi 104. Katika hotuba yake Rais Kikwete aliwapongeza wahitimu hao kwa kutunukiwa vyeo hivyo, na pia aliwataka maafisa wa Jeshi hilo wafuate sheria kwa wawatendea haki Mahabusu na Wafungwa katika magereza nchini.
Kikosi Maalumu cha Ukakamavu cha Jeshi la Magereza (KMKM) kikimuonesha Rais Jakaya Kikwete na wageni waalikwa (hawapo pichani)  jinsi kikosi hicho kinapokuwa kazini wakati wanapopambana na wahalifu wa aina tofauti. Rais Kikwete aliyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi hilo pamoja na kuwavisha vyeo vya Mrakibu Msaidizi wahitimu 104 wa jeshi hilo katika sherehe iliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha Gwaride la Wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi la Magereza kikipita mbele ya Jukwaa Kuu kutoa heshima kwa mgeni rasmi Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani) katika sherehe ya ufungaji wa mafunzo hayo ya Cheo cha Mrakibu Msaidizi  yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam. Wahitimu 104 walivishwa cheo hicho. Ufungaji wa mafunzo hayo yalienda sambamba na Siku ya Magereza ambapo Rais KIkwete alikagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na jeshi hilo nchini.
Rais Jakaya Kikwete akiiangalia bilinganya wakati alipokuwa anatembelea mabanda yenye bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Jeshi la Magereza nchini. Rais Kikwete alitembelea maonyesho hayo maalumu yanayofanyika kila mwaka katika Siku ya Magereza, mara baada ya kuyafunga mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi hilo pamoja na kuwavisha vyeo vya Mrakibu Msaidizi wahitimu 104 wa jeshi hilo, katika tukio lililofanyika Uwanja wa Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Kilimo wa Jeshi hilo, Yesaya Kitundu. Wapili kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, na anayefuata ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick. 

Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.