Wednesday, September 2, 2015

Kamishna Jenerali wa Magereza afungua rasmi kongamano la wasaidizi wa kisheria magerezani mkoani Morogoro

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa hotuba kwa Maofisa Wasaidizi wa Kisheria Magerezani kwenye ufunguzi wa Kongamano la Wasaidizi wa Sheria lililofadhiliwa na Shirika la Envirocare ambapo Kongamano hilo litafanyika kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 2, 2015 Mkoani Morogoro.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo ambao ni Maofisa wa Jeshi la Magereza kutoka Mikoa Mitano Tanzania Bara(Dar es Salaam, Tanga, Arusha, Kilimanjaro na Morogoro) wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi ambaye ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani).
Meza Kuu wakimsikiliza Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani - Jeshi la Polisi, Kamisheni ya Upelelezi, Mrakibu wa Polisi Emmy Mkonyi(hayupo pichani). Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kwa Umma kutoka Wizara ya Sheria na Katiba, Bw. Joseph Ndunguru(kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema(katikati) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema akitoa maelezo mafupi ya lengo la Kongamano hilo ambalo ni kutoa msaada wa Kisheria Magerezani ili kupunguza Msongamano Magerezani.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akimpongeza baada ya kukabidhi cheti cha kuhitimu Mafunzo ya Wasaidizi wa Kisheria Magerezani kwa mmoja wa Washiriki wa Kongamano hilo linalofanyika Mkoani Morogoro.
Mwandishi wa Habari wa ITV, Bi. Devotha Minja akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja mara baada ya ufunguzi rasmi wa Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria katika Viwanja vya Ukumbi wa CCT uliopo Mkoani Morogoro(wa pili kulia) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema(kulia) ni Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi - Jeshi la Polisi, Mrakibu wa Polisi Emmy Mkonyi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(katikati) walioketi akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria kutoka Mikoa Mitano ya Magereza Tanzania Bara(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunula(wa pili kulia) ni Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kwa Umma, Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Joseph Ndunguru(wa kwanza kushoto) ni Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi - Jeshi la Polisi, Mrakibu wa Polisi, Emmy Mkonyi(wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).