Saturday, January 30, 2016

Naibu katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi, balozi Yahya aridhishwa na uzalishaji wa mifugo katika shamba la mifugo la gereza Mtego wa Simba, mkoani Morogoro

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya, akisalimiana na maafisa wa Jeshi la Magereza alipotembelea  Gereza la uzalishaji mifugo Mtego wa Simba lililopo Mkoani Morogoro.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya, akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Gereza la uzalishaji mifugo Mtego wa Simba. Kulia ni Mkuu wa Gereza hilo Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Omari Msepwa.
Mtaalamu wa Mifugo katika shamba la uzalishaji mifugo katika Gereza la Mtego wa Simba Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Constatus Magori akitoa maelezo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya( kushoto)alipotembelea Gereza hilo Januari 30, 2016 kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji  zinazofanywa gerezani hapo.
Kundi la ng’ombe wa maziwa wanaofugwa katika shamba la uzalishaji mifugo Gereza la Mtego wa Simba wakiwa malishoni kama wanavyoonekana katika picha.
Mtaalamu wa mifugo katika mradi wa ufugaji kuku wa mayai na nyama uliopo Gereza Kuu la Wanawake Tanzania, Kingolwira, Sajeni taji Sarah Kabunda akitoa maelezo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya(kushoto) alipotembelea Gereza hilo Januari 30, 2016 kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji  zinazofanywa gerezani hapo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya(wa pili kutoka kushoto), akiangalia mojawapo  ya mashuka yanayofumwa kwa ustadi mkubwa na wafungwa wa kike katika  Gereza Kuu la Wanawake Tanzania- Kingolwira, lililopo mkoani Morogoro.

(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)