Thursday, February 4, 2016

Kamishna jenerali wa magereza John Casmir Minja ashiriki maadhimisho ya siku ya sheria nchini, jijini Dar

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Othman Chande akiwaongoza Maandamano ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuelekea katika hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika leo Februari 04, 2016, Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(katikati) akifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli(hayupo pichani). kulia ni Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Poilisi, Abdulrahmani Kaniki(kushoto) ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Valentino Mlowola.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitoa hotuba yake fupi katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika leo Februari 04, 2016, Jijini Dar es Salaam.
Wageni Waalikwa na Wadau mbalimbali wa Sekta ya Sheria wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Othman Chande akitoa hotuba yake fupi katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika leo Februari 04, 2016, Jijini Dar es Salaam.
Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama/Wawakilishi wa Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama waliohudhuria Maadhimisho hayo ya Siku ya Sheria nchini(wa pili kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali, Kidini na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama(waliosimama msatari wa nyuma)katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika leo Februari 04, 2016, Jijini Dar es Salaam(wa nne kushoto) ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Othman Chande(wa tatu kushoto) ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Harrison Mwakyembe(wa nne kulia) ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. TULIA Mwansasu.
Bendi ya Jeshi la Poilisi ikiongoza Maandamano ya Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika leo Februari 04, 2016, Jijini Dar es Salaam

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).